Floyd Mayweather ni mwanamichezo wa 3 kufikia ubilionea - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Thursday, 31 August 2017

Floyd Mayweather ni mwanamichezo wa 3 kufikia ubilionea

Floyd "Money" Mayweather katika moja ya mapambano yake.

Jumapili ya Agost 27, 2017 Floyd Mayweather alishinda mpambano uliobatizwa jina la Pigano la Pesa “The Money Fight” na sasa ameingia kwenye uwanja mpya wa klabu ya wanamichezo mabilionea “The Billionaire Athlete Club” kwa thamani ya dola ya Marekani.

Mayweather anatarajia kuweka kibindoni kiasi cha $300 milioni kutoka kwenye mpambano wake dhidi ya Conor McGregor, mkali wa mchezo wa mapigano mchanganyiko (MMA) aliyechakazwa raundi ya kumi ya mpambano huo. Pesa hii ikithaminishwa kwa Shilingi ya kitanzania tarakimu yake inasomeka ni 672,300,000,000.00, yaani bilioni mia sita sabini na mbili na milioni mia tatu.

Floyd Mayweather vs Conor McGregor kwenye mpambano wa pesa Agosti 27, 2017.

Bondia huyu mwenye mbwembwe nyingi sasa anajivunia rekodi yake ya kushinda michezo 50-0, ameshajikusanyia jumla ya $700 milioni kutokana na kazi yake hii ikiwemo malipo ya haki za matangazo ya televisheni, mauzo ya tiketi na malipo ya kupigana ulingoni.

Leonard Ellerbe, promota mkuu wa Mayweathe anasema “baada ya pambano hili, Mayweather anaungana na mkali wa basketball Michael Jackson na mwamba wa mchezo wa golf Tiger Woods na kuwa ni wanamichezo watatu pekee waliofanikiwa kujitengenezea kiasi cha pesa kisichopungua $1 bilioni.

“Sidhani kama amewahi kuikosea kazi yake,” aliongeza Ellerbe.

Jordan alitengeneza zaidi ya $93 milioni kwa kazi yake, kulingana na maelezo ya kampuni ya Spotrac ya utafiti wa mishahara. Hata hivyo bado anamikataba mingine kadhaa ikiwemo ule wa kudumu na kampuni ya Nike.

Mikataba hii imemuwezesha kuingia kwenye kilabu cha mabilionea, na hata  umiliki wake wa Charlotte Hornets (klabu ya mpira wa kikapu USA). Mwaka 2015 kwa mara ya kwanza aliorodheshwa miongoni mwa mabilionea kwenye gazeti la Forbes.

Tiger Woods pia aliwahi kuwemo kwenye orodha hiyo. Mwaka 2009 Forbes ilikadiria kuwa ushindi na mikataba yake mingi inamfanya Woods kuwa bilionea. Lakini akiba yake kwa miaka ya hivi karibuni imeporomoka kwakuwa hajaweza kushinda mashindano yoyote tangia mwaka 2008.

Na ile kashfa kubwa ya kingono imesababisha wadhamini kumtema. Forbe inakadiria kuwa utajiri wa Woods kiasi $740 milioni mwaka 2016.

Mwanamichezo mwingine anayenekana kuelekea huko pia ni LeBron James. Nyota huyu wa kikapu (NBA) anamwelekeo mzuri ameshajipatia mamilion ya dola kazi yake kama mchezaji na kusaini mikataba mbalimbali ikiwemo ule wa kudumu na kampuni ya Nike tangu mwaka 2015.

Mayweather akiwa katika pozi kwenye gari lake la thamani kubwa


1 comment:

Post Bottom Ad