MATUKIO 15 YA AJABU KABISA KUHUSU MIKE “IRON” TYSON - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Wednesday, 20 September 2017

MATUKIO 15 YA AJABU KABISA KUHUSU MIKE “IRON” TYSON


Ni nini ambacho bado hujasikia kuhusu bondia huyu bora kabisa aliyepata kutokea duniani?
Mbabe huyu mwenye miaka 50 anafahamika vyema karibu na kila mtu kama mwamba wa ngumi za uzito wa juu, na ile tattoo yake ya jichoni. Pia kwasasa anafahamika kupitia tasnia ya filamu na anaeleweka kuwa si mtu wa kubishana naye hovyo hovyo. Mbali ya haya yote ikumbukwe kuwa mwamba huyu ameshahusika kwenye matukio mengine ambayo ni ya ajabu sana kwa mtu mwenye akili timamu akiyatafakari.
Swali langu ni je, unapata taswira gani unapomfikiria Mike Tyson? Kwamba ni mtu wa aina gani kwenye kujenga hoja? Anavutia, mpole, mcheshi? Sahau namna yoyote ufikiriavyo kuhusu Tyson alivyo. Hamishia akili yako hapa na upate simulizi za kweli kumhusu na mambo kadhaa aliyopata kuyapitia maishani mwake.
Katika Makala moja ya New York Magazine, Mike Tyson alisema hivi kuhusu maisha yake ya awali.
Kuna watu wanaweza kusoma mambo ninayozungumza na wakanihukumu kama mtu mzima, wacha tu niitwe mharifu, lakini ikumbukwe kuwa mambo hayo niliyafanya miaka 36 iliyopita. Nilikuwa bado mtoto mdogo na nilikuwa natafuta upendo ambao sikuupata sehemu nyingine zaidi ya mitaani. Mtaa ndiyo ulikuwa elimu yangu pekee na watu wa mtaani ndiyo walikuwa walimu wangu.”
Kwa jinsi Tyson alivyozidi kukuwa, hakika akapevuka na kuwa binadamu wa namna yake duniani.
Je, ni kwamba Tyson alijihusisha na maovu katika maisha yake, au ni kwakuwa alizungukwa na mazingira yaliyomlazimu kufanya uovu? Hili ndilo linazua mjadala mzito, au tuseme kwamba watu aliokuwa anashinda nao muda mwingi na matendo yake ndiyo yalipelekea yeye kuwa hivi alivyokuwa. Au ni makosa yake mwenyewe?
Weka akilini mwako mbali ya kwamba simulizi hii imebeba matukio mengine ambayo ni ya ajabu kueleza, lakini ni ukweli kutoka kwa Mike Tyson mwenyewe.
15. Tyson Anamshambulia Mbeba Takataka

Wakati akiwa bado mdogo, Tyson alikuwa na afya njema, mwenye nguvu sana na mbabe. Kuna siku alimwona mbeba takataka akiweka mzoga wa njiwa (Tyson alimpenda sana njiwa huyo) kwenye pipa. Tyson alimfuata na kumtandika ngumi kali kwa mkono wa kulia iliyompeleka mtu huyo chini na kuumia sana. Yeye alitaka kumuhifadhi njiwa huyo kwenye boksi zuri kama sehemu ya heshima na upendo. Tyson anasimulia.
Niliacha ile boksi kwenye tundu ya kufugia njiwa na nikaingia ndani kufuata kitu fulani niliporudi nikaona mtu wa takataka anatia ile boksi yangu kwenye crusher na kuondoka zake. Nilimkimbilia kadiri alivyokuwa anatokomea kuelekea kwenye hekalu moja, kwa mkono wa kulia nilimchapa konde takatifu akaanguka chini na kuanza kutapatapa kama kitoto kichanga kinavyojikongoja.”
Cha ajabu mwaka 1996 Tyson alisimulia tukio hili kwa kujiamini kabisa kanakwamba  alifanya tukio sahihi na lenye maadili.

14. Miaka Mitano Bila kushiriki Ngono

Ni kweli kwamba Mike “Iron” Tyson kitendo cha ngono mwaka 1981 – 1986.
Alichukua maamuzi ya kuelekeza akili na nguvu kwenye mchezo wa masumbwi ili awe bondia bora kabisa ambaye hajapata kutokea duniani, kwahiyo hakutaka kukumbana na kizuizi chochote njiani. Kwa namna fulani alifikiri kwamba kushiriki ngono kungemfanya awe dhaifu. Ni hadithi ya wake wa kale kwamba kushiriki kitendo cha ngono kabla kupigana hushusha kiwango cha testosterone mwilini mwa mwanaume na hivyo kuwa dhaifu.
Tyson ni mwanaume mwenye mbinu za kipekee, na huwia vigumu kuuliza mikakati ya ushindi wake wote alioupata.

13. Kilevi Wakati wa Mpambano

Wakati wa mpambano wake dhidi ya Lou Savarese, mwezi june mwaka 2000, Tyson alipigana huku akiwa amelewa bangi na cocaine kwa wingi na bado aliweza kushinda. Aliweza kukwepa vipimo kwa kuwasilisha sampuli ya mkojo ya uongo. Anasema kwamba amepigana mapambano mengi tu akiwa amelewa na mengine hawezi kuyakumbuka.
Cha ajabu zaidi huo ndiyo ulikuwa mpambano wake wa kurejea kazini na kumuimarisha kama mtu makini kabisa ulingoni, na kama kuna mtu anayeweza kupigana ulingoni akiwa tilalila basi huyo Mike Tyson pekee.
12. Mkojo Feki Kwenye Kipimo Cha Matumizi ya Dawa
Mike Tyson na promota Frank Warren

Katika wasifu wa Mike Tyson anaeleza mbinu zake za kukwepa vipimo vya dawa mwilin. Anasema kuwa alitumia uume wa uwongo uliojazwa mkojo wakati wa vipimo. Tyson anadai mwaka 2000 wakati wa mpambano wake THC alikutwa na kiwango cha dawa mwilini, kwasabuabu mtu aliyepewa jukumu la kubeba ule uume bandia alisahau siku hiyo.
Promota wa mapambano mengi ya Tyson, bwana Frank Warren, anadai kuchukizwa sana na simulizi hizi.
Nachukizwa sana na hadithi hizi za kupuuzi, alipopigana hapa alifanyiwa vipimo na UK Sport, ambao hufanya vipimo vyote vya mabondia na hakuna chochote kilichoonekana kwenye mfumo wake wake wa damu.” Anasema bwana Warren".
Anaendelea kusema kuwa haiwezi kuwa kweli bali Mike Tyson anayasema haya ili kuuza kitabu”.

11. Anamtandika Makonde Don King

Mike Tyson na promota wake Don King hawakuwa sawa kama vile unaweza kudhani. Mwaka 2003 Tyson aliruka na ndege yake binafsi kwenda Miami – Florida kuonana na King. Tyson akaanza kumkong’ota ngumi na makonzi King aliyekuwa akiendesha gari kuelekea sehemu fulani kufanya mazungumzo yao.
Tyson anakiri kuwa walikuwa na mahusiano mazuri na King. Lakini alimchukia tu kwasababu ambayo bado hajaiweka wazi lakini inawezekana sababu ikawa ni zile $400 mil ambazo zilitoweka ghafla uweponi mwa Tyson.
Hata hivyo tuelewe tu kuwa kupigwa kichwani na mtu kama Tyson maumivu yake si madogo, mbali ya hayo, hakika akikukong’ota sehemu yoyote mwilini ni lazima uugulie kwa sana.

10. Amtundika Mimba Afisa  wa Gereza

Ndani ya gereza kuna umm, upuuzi mwingi tu hutokea humo. Tyson alikuwa alipangiwa kuonana na mshauri (counselor) wa gereza mara moja kila juma, na hatimaye akawa na mahusiano ya kingono mara tatu kwa siku. Mambo yakaendelea kuwa hivyo mwishowe yule afisa akashika mimba, Tyson ananukuliwa akisema “nilimpa mimba afisa jela nilipofungwa gerezani, lakini hakupata mtoto.”
Tyson anaendelea kusema kwamba mambo haya yanatokea sana gerezani kama kitu cha kawaida. Lakini hili si jambo linalofanya watu watafakari sana juu ya tabia yake, isipokuwa ni juu ya maadili yake na ni nani aliyemfunza maadili hayo? Huyu ndiyo Tyson, hakika hakufunzwa na mtu bali alijifunza mwenyewe hata angali mtoto mdogo kabisa.
9. Mitch Green

Mwaka 1988, Mitch Green, bondia wa uzani wa juu alikutana na Tyson kwenye kituo cha biashara (shopping mall). Green alishatwangwa na Tyson kwenye mpambano kwahiyo akasema anataka mpambano mwingine. Lakini badala ya kufanya makubaliano ya tarehe ya mpambano Tyson akaanza kumtandika Green hadharani, bila kujali kuwa Green alikuwa bado anamajeraha kadhaa mwilini. Green ndiye aliyeanza kumkabili Tyson kwasababu alidai kuwa Don King bado hajalimpa stahiki zake za mpambano wao wa kwanza. Hatimaye mahakama ya kiraia ikaamuru Tyson kumlipa Mitch Green kiasi cha $45,000 kwa madhara ya kushambulia hadharani.
Pamoja na kwamba Tyson alimshushia kipigo kizito bondoa huyo na kumwonyesha huo ndiyo mpambano wa marudiano aliouhitaji kwa kumchakaza uraini. Kipigo hicho cha mbwa mwizi kilipelekea macho ya bwana Green kuvilia damu na kusababisha asiweze kuyafungua tena.

8. Hongo kwa Afisa wa Zoo

Mwaka 1989 tyson alianikiwa kumhonga mtunza bustani ya wanyama na kuachiwa atembee bustanini humo kwa saa kadhaa akiambatana na mkewe. Alikuwa eneo la masokwe Mike Tyson alijaribu kumhonga mtunza bustani hiyo kiasi cha $10,000 ili asizuiwe kwenda kuingia kwenye cage akapigane na sokwe aliyekuwa anamshambulia mwenzie. Shukurani kwa huyo mtunza bustani kwani alikataa kumruhusu Tyson asije raruriwa na mnyama huyo mwenye ghadhabu. Ubabe wake ni kwa binadamu wenzie tu na siyo wanyama wakubwa kama sokwe hahahahaaa…..hao ni viumbe wengine kabisa.
Mtunza bustani alishafanya kosa kumruhusu Tyson kuzurura bustanini humo na kamwe hakutaka tena kurudia kosa kwa kumwachia akapigane na mnyama.

7. Akong’ota Washabiki Wake

Mike Tyson anadai kuwa ananmna yake ya kukabiliana na washabiki wake. Hata wale waliomba saini yake. Tyson anakiri amewahi kuwatandika makonzi na makofi mashabiki wake waliozidisha midadi.
Mwaka 2003, Tyson alivamiwa ghafla na washabiki wawili kwenye lango kuu la hoteli anadai kwa kuendeshwa na akili ya ulevi wa cocaine aliwakimbiza akamchapa mmoja konde la uso lilipelekea kupoteza fahamu, na yule mwingine akaokolewa na mtumishi wa hotelini hapo baada ya kutoa taarifa kwa walinzi.
Hii ndiyo tabia ya Tyson ni mkorofi na humshambulia mtu yeyote anayemsababishia usumbufu.

6. Awekewa Bastola Kichwani

Mwaka 1983, Tyson alikuwa bado yuko kwenye rika la balehe, mwalimu wake Teddy Atlas alimwekea bastola kwenye paji la uso. Atlas alidhani kwamba Tyson alikuwa na mahusiano ya kingono na binti yake wa miaka 11, akamuonya Tyson kuwa asijaribu kucheza na familia yake au la atakufa. Teddy akafutwa kwenye chama cha ngumi cha Catskill baada ya tukio hili.
Baada ya siku kadhaa Tyson alidai kuwa aliwahi kushika makalio ya binti yake Yeddy mara moja. Tyson huwa hakatai jambo ambalo amelifanya, lakini aliingiwa na woga baada mzee huyo wa kizungu kumwelekezea bastola ile kichwani, hasa ukizingatia wakati huo kesi ya ubaguzi wa rangi ilikuwa imeshika moto nchini humo.
Teddy akaendelea kuwafundisha mabondia wengine na akawa mtangazaji wa michezo. Sidhani kama baada ya hapa Tyson na Teddy walichekeana tena, hapana siyo rahisi kabisa.

5. Miujiza na Uchawi

April 1, 1992 wakati Tyson akiwa gerezani kutumikia adhabu yake ya kesi ya ubakaji, alijaribu kutafuta mbinu mbalimbali za kupunguza kifungo chake. Tyson alimsikiliza mchawi mmoja na akafanya mambo fulani  kufuatisha maelekezo. Akaweka $500 mtungi wa glasi (sifahamu aliutoa wapi wakati akiwa humo ndani), akakojoa humo na kuosha mikono yake kwa kutumia mafuta ya aina mbalimbali na maji. Pia akanywa kinyaji cha detox baada ya kufuatisha maelekezo yote ya awali ya uchawi huo.
Pia alifanya uchawi mwingine wa kutupa yai sakafuni na kupiga uyowe huku akitamka neno “I’m free”. Nadhani kuanguka na kupasuka kwa yai kuliashiria kuwa Tyson kutoka kwake gerezani miaka mitatu baadaye. Huenda ni kweli ulozi huu ulikuwa ni sehemu muhimu ya kuachiwa kwake huru, hakuna ajuaye!!!!!

4. Alipowehuka akiwa na Steve-O

Bila shaka sasa umetambua kwamba Mike Tyson alikuwa mpenzi sana wa kubwia unga. Wakati wa intavyuu moja na GQ alifinguka kuwa dawa za kulevya zilichochea kukuwa kwa urafiki baina yake na huyu bingwa wa ngumi mstaafu. Unaweza usiamini ukiambiwa kuwa hawa jamaa walijifungia bafuni na wakabwia cocaine gramu 5.5. na kali zaidi ni pale Tyson alipoamua kutoa tumbaku yote kwenye sigara na kuijaza cocaine. Ingawa walikuwa pamoja humo bafuni lakini alitumia cocaine yote peke yake.

3. Akiri Kufanya Maovu ya Zaidi ya Ubakaji

Mwaka 1991, Tyson alidai kwamba katika maisha yaake ameshafanya mambo matano–saba ambayo ni maovu zaidi ya kumbaka mtu.
Inawezekana vipi kufanya mambo hayo matano mpaka saba ambayo ni mazito zaidi ya ubakaji? Kuna jambo gani lingine ambalo ni zito zaidi ya hilo? Labda tuseme kuua mtu ni tukio baya na zito zaidi, au labda kuiba mwili wa marehemu. Kwakweli hili ni japo la hatari sana ambalo halifai hata kulijadili.
Mara kadhaa ameshaliongea hili kwamba ni kweli mambo mengi maovu sana na hajawahi kuonekana kujutia lolote. Hata kama anaonyesha kusikitishwa na matukio hayo hautaweza kuamini kuwa anayesimulia ndiyo mtenda maovu hayo. Si jambo rahisi mtu kusema kuwa umembaka mtu fulani, kumbaka mtu ni jambo la hatari na haipendezi mtu kuutenda uovu huo.

2. Awatandika Machangudoa Saba

Mwaka 2009, Tyson aliwazabua machangudoa; siyo mmoja ama wawili, alitandika makofi wadada saba. Alikuwa amelewa usiku huo, kama watu wengine na akawa kama kavurugwa akili. Alikuwa amejipigilia morphine, cocaine na akashusha na vodka. Akadhani madada poa wangeweza mchomolea wallet yake, kwahiyo akang’aka.
Nilikuwa nipo sehemu yenye giza. Kulikuwa kuna namna ya ujanja nilidhani nafanyiwa, kwasababu kuwaachia hata senti moja” anasimulia Tyson.
Maelezo yake yanafanya aonekane mwehu. Mbali ya kuwashambulia wanawake hao saba na kuwatoa na damu na pia kuwaachia makovu, anadai kwamba siku hiyo alikumbana na shetani halisi katika mwake akidai kuwa majini na maruhani yanamuwinda sana.

1.     Brad Pitt vs Mike Tyson

Mwaka 1988, kuna siku Tyson alikuwa anenda nyumbani kwa mtalaka wake bila kumtaarifu. Akiwa anaendesha taratibu kuelekea kwenye parking ya Robin Givens, akaona hakukuwa na gari hivyo akilini mwake akajua hapakuwa na mtu pale nyumbani.
Akatembea mpaka mlangoni akasimama kwa mkono ukiwa kwenye kengele ya mlango, akashtushwa na muungurumo wa gari kabla hajapiga hatua ya kuondoka eneo lile, alipoitaza parking akiona gari ya mcheza sinema Brad Pitt akiwa na mkewe Robin. Pitt anasimulia kwamba hili lilikuwa ni tukio la kutisha sana, alihisi kama amekutana na mzimu.
Siku moja naenda nyumbani kwake kumsabahi kwa mara nyingine lakini nyumbani hakukuwa na mtu, sasa natoka naona mtu huyu hapa anakokotana Brad Pitt wakirejea, nilipatwa na uchungu sana. Wakati huo hakuwa Brad Pitt huyu ……kalikuwa ni kabichi fulani tu…..nikamtazama tu, alikuwa anautumia mwili wake kujipatia kipato au kitu fulani, mi sielewi……..lakini tambua tu kuwa jamaa kalikuwa kazurizuri hivi.” Anasimulia Tyson.
Cha ajabu Tyson hakumshambulia Pitt, alijivuta taratibu na kuondoka nyumbani kwa Robin. Haijafahamika mpaka sasa kwanini Pitt hakukong’otwa kama watu wengine waliojileta kwenye uso wa chuma “Mike Tyson”.



Makala hii imetafasiriwa na Davis Mwakalosi kwa hisani ya jarida la The Sportster la Marekani, unaweza kuwasiliana na mwandishi huyu kwa email sportstz17@gmail.com

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad