ARSENE WENGER KATIKA CHANGAMOTO YA MIKATABA YA WACHAZAJI WAKE - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Saturday, 23 September 2017

ARSENE WENGER KATIKA CHANGAMOTO YA MIKATABA YA WACHAZAJI WAKE

Na Davis Mwakalosi



Alexis Sanchez na Mesut Ozil inawezekana wakatembea zao mwakani, na pia Aaron Ramsey na mapanki Danny Welbeck wakaondoka msimu unaokuja.
Ramsey na Welbeck wakati wa mazoezi eneo la uwanja wa timu yao ya Arsenal

Bila kujali kwamba mikataba ya Welbeck na Ramsey inaelekea ukingoni mzee Wenger bado amesimamia msimamo uleule wa kutokubadili sera za mikataba ya klabu yake ya Arsenal.

Arsenal wajiandae tu kisaikolojia kuwaachia Ozil na Sanchez kwakuwa wote wawili mikataba yao inafika ukomo ndani ya muda mfupi ujao hivyo kunauwezekano mkubwa wakaondoka na klabu isiambulie hata senti.

Mwingine ni Jack Wilshere ambaye amebakiza chini ya mwaka mmoja, ikumbukwe kuwa Alex Oxlade Chamberlain aliuzwa kwenda Liverpool fc akiwa amebakiza miezi 12 tu kumaliza mkataba na Arsenal.
Arsenal fc wanaonyesha dhahiri watakosa huduma ya Sanchez na Ozil msimu ujao bila ya kuambulia hata senti moja.

Jirani zao, yaani Tottenham Hotspurs wameshapata somo na sasa wamekuwa macho kutokuruhusu mikataba ielee elee chini ya miaka miwili, hawatasau maumivu ya kumpoteza beki kisiki Sol Campbell aliyeondoka bure kuelekea Kaskazini mwa London kwa mpinzani wao mkubwa Arsenal mwaka 2001.

Ramsey na Welbeck wote wana miaka 26 na wamebakiza mikataba ya miaka miwili.
Ramsey analipwa pound 100,000 kwa wiki, alifunga bao la ushindi wa fainali za kombe la FA mwezi May na bado ni mchezaji muhimu sana kwenye kikosi cha kwanza cha Arsene Wenger.

Welbeck amepambana na majeraha yalimuweka nje muda mrefu na kufanikiwa kujiimarisha miongoni mwa wachezaji muhimu wa kilabu hiyo. Mmshambuliaji huyu wa kiingereza analipwa pound 70,000 kwa wiki atakuwa nje ya uwanja hadi October kutokana na jeraha la kinena alilopata wiki iliyopita kwenye michuano ya kimataifa.

Wenger anasisitiza kuwa hana hofu baada ya kina Sanchez kuwa katika mpango wa kuongezewa mikataba yao bila kuifanyia mabadiliko ya kisera.

“Hakuna kabisa” aliongea kuelekea mchezo wao wa jumatatu dhidi ya West Brom. “Kiasi cha pesa cha uhamisho na kile cha mkataba anachotaka mchezaji, utaona ni wachezaji wengi wapo kwenye mwaka wa mwisho mikataba yao.”

“Kwahiyo utajikuta upo kwenye sehemu ambayo inatakiwa uongeze mkataba usioumudu malipo yake au la utaacha tu mwaka umalizike.” Alisema Arsene Wenger.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad