Na Davis Mwakalosi
Miaka 25 baada ya
kuundwa kwa ligi kuu Wingereza (English
Premier Leagu), huu ni mzigo kamili wa matukio ya ajabu yaliyotokea ambayo kwa
hakika hukuwahi kuyafikiria wala
kuyasikia kabla ya leo.
![]() |
| Hii ndiyo Ligi yenye umaarufu kushinda zote duniani |
01.Ni
wachezaji wawili tu waliofunga penati kwa miguu kwa miguu yote miwili, Bobby Zamora na Obafemi
Martins.
![]() |
| Bobby Zamora |
02.Ryan Giggs
ndiye mchezaji aliyefanyiwa sub nyingi kuliko mwingine yeyote, (134).
![]() |
| Ndiyo ni kweli hatuwezi kukataa kwamaba amecheza michezo mingi kwakuwa ametumia muda wake wote EPL, lakini amejiongezea rekodi yake nyingine ambayo ni hii. |
03.Mario Baloteli
amepiga pasi ya goli moja tu kwa Sergio Aguero
kwenye EPL katika mchezo baina ya Man City
na Queens Park Rangers.
![]() |
| Sahau habari ya Man City kunyakuwa ubingwa wa ligi msimu huo, lakini ukumbuke tu ya kwamba bao hili la Sergio Aguero kwenye mchezo dhidi ya QPR lilitokana na pasi ya Mario Baloteli. |
04.Wayne Rooney,
Gareth Bale na Kevin
Davies ni wachezaji pekee waliofunga, kutoa pasi ya goli na kujinga
katika mchezo mmoja.
![]() |
| Wayne Rooney akijifunga kwenye mchezo wa Man U dhidi ya Stoke City mwaka 2012 |
05.Man U
ni klabu ambayo haijapoteza mchezo Old Trafford baada kuongoza kipindi cha
kwanza cha mchezo huo.
![]() |
| Sir Alex Ferguson, shukurani nyingi ziende mzee huyu mwenye rekodi kibao kwenye timu hiyo |
06.Alan Shearer
amekosa penati nyingi zaidi kwenye EPL (11), lakini pia ndiye aliyfunga nyingi
kuliko wote (56).
![]() |
| Alan Shearer akishangilia bao msimu wa 2002/03 |
07.Msimu
wa 2015/16 ilikuwa ni mara ya kwanza kwa West Ham
kufunga magoli mengi kuliko msimu wa 1985/86.
![]() |
| Msimu wa 2015/16 ulikuwa ni mzuri kwa West Ham kiasi cha kufungua shampeni na kulipua mafashifashi |
08.Kipa
mstaafu wa timu ya taifa ya Wingereza Paul Robinson,
ameshafunga, ametoa pasi ya mwisho na kufunga penati kwenye EPL. Ndiye mwenye
pasi za mwisho (5) nyingi kuliko golikipa mwingine yeyote kwenye ligi hiyo.
![]() |
| Paul Robinson |
09.James Milner
amefunga magoli 47 kwenye EPL na kila anapofunga basi timu yake ya Liverpool haikupoteza mchezo.
![]() |
| James Milner akiwa Liberty Stadium kwenye baina ya Burnley na Liverpool |
10.Ni
wachezaji watatu pekee waliozaliwa baada ya ligi hiyo kuitwa English Premier
League (August1992) wamefanikiwa kupiga hat-tricks, Raheem
Sterlin, Harry Keane na Romero Lukaku.
![]() |
| Harry Keane na moja ya mipira yake mingi aliyoipata baada ya mchezo kumalizika |
11.Mtu
pekee aliyezaliwa kabla ya mwaka 1960 na kufunga hat-trick kwenye English
Premier League ni Gordan Strachan.
![]() |
| Raia wa Scotland, Gordon Strachan amezaliwa February 9, 1957 na kuchezea Leeds United na Coventry City baada ya mfumo kubadilishwa na kuitwa English Premier League. |
12.David
(x14) na James (x11) yalikuwa majina yaliyozoeleka sana kwenye English Premier
League msimu wa 2010/11, lakini haikuwa hivyo kwa golikipa David James, kwani hakufanikiwa kucheza hata
mchezo mmoja.
![]() |
| David James |
13.Msimu
wa 2014/14, George Boyd akawa mchezaji wanne
kuchezea timu mbili ambazo zote zilishuka daraja kwenye msimu huo huo wa ligi,
wengine ni Mark Robins 1994/95, Steve Kabba 2006/07 na David
Nuget 2009/10.
![]() |
| George Boyd wakati akiitumikia timu ya Burnley kwenye msimu wao mbovu. |
14.Msimu
wa 2014/15 Leicester City ilikuwa ni timu iliyokaa mkiani mwa msimamo wa ligi
kwa muda mrefu zaidi bila kushuka daraja kuliko katika historia kwa jumla ya siku
142.
![]() |
| Claudio Ranieri |
15.Cezar Azpilicueta
(2016/17), Wes Morgan (2015/16), John Terry (2014/15) na Garry Pallister (1992/93)
ni wachezaji pekee waliocheza dakika zote msimu husika wa ligi na kubeba
ubingwa.
![]() |
| John Terry |
16.Peter Crouch
amefunga mabao mengi kwa kichwa (50) zaidi ya 16 yaliyofungwa na timu
alizochezea kwneye English Premier League.
Pic
17.Nuri Sahin
(mchezaji wa zamani wa Liverpool) amecheza michezo mingi bila kuwa sub kuliko
mchezaja yeyote kwenye michezo ya English Premier League (7).
![]() |
| Peter Crouch akifunga la kichwa dhidi ya Liverpool |
18.Richard Wright
amecheza michezo 12 tu kwenye Enlgish Premier League, michezo (12) akiwa Arsenal
na (0) akiwa Man City, lakini ameshasherehekea ubingwa wa ligi mara mbili.
![]() |
| Richard Write mwenye bahati ya mtende, bahati haba ya kucheza lakini amebeba ubingwa mara mbili. |
19.Lago Aspas
amepiga mipira mingi ya kona hovyo kuliko akipiga kawaida.
![]() |
| Lago Alpas mfalme wa kona mbovu |
20.Msimu
wa 1997/98, Andy Roberts alicheza michezo 37
kwenye English Premier League na kati ya hiyo minne aliumana na Arsenal fc
(miwili akiwa anaitumikia Crystal Palace na miwili mingine akiwa Wimbledon).
21.Terry Connor,
ndiye kocha pekee kwenye English Premier League aliyepata kufundisha vilabu
zaidi ya kumi bila kuchukua ubingwa hata mmoja.
![]() |
| Masikini mwe, Terry Connor |
22.Msimu
wa 2016/17, Hull City imekuwa ni timu ya
tatu kuwahi kushika nafasi tatu za juu na msimu huohuo kushuka daraja. Nyingine
ni Charlton 1998/99 na Bolton Wanderers 2011/12.
![]() |
| Hull City wakishangilia bao kwenye mchezo dhidi ya Leicester City |
23.Ni
wachezaji wawili tu waliopiga hat-tricks kwa kichwa kwenye michezo ya English
Premier League: Duncan Ferguson wa Everton
(dhidi ya Bolton Wanderers, Dec 1997) na Solomon
Rondon wa West Bromwich (dhidi ya Swansea Dec 2016).
![]() |
| Solomon Rondon |
uchambuzi huu umekujia kwa hisani ya mtandao wa Mirror wa Wingereza























No comments:
Post a Comment