Arsenal wanamfikiria striker wa AC Milan kama mbadala sahihi wa Sanchez - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Tuesday, 17 October 2017

Arsenal wanamfikiria striker wa AC Milan kama mbadala sahihi wa Sanchez

PIA: Gunners wakwazika maamuzi ya FA juu ya tukio la Richarlison.


Arsenal wanaweza kumsajiri striker wa AC Milan, Andre Silva wakati wa majira ya joto.
Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Portugal alihusishwa na kwenda Emirates kabla hajakamilisha uhamisho ulioweka record San Siro.
Dalili hainyeshi maendeleo mazuri kwa Milan kiuchumi na hata kisoka kiasi kwamba wameanza vibaya kwenye ligi ya klabu bingwa Ulaya.
Kulingana na taarifa ya The Sun, Silva atakuwa miongoni mwa wachezaji ambao watanyakuliwa na timu nyingine iwapo Vincenzo Montella atashindwa kuisimamia timu vyema.

Mchezaji wa AC Milan, Andre Silva akiwa kazini.
Wakati huohuo FA imethibitisha kwamba mshambuliaji wa Watford, Richarlison hataadhibiwa kwa udanganyifu uliopelekea kupata penalty iliwapatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Arsenal.

Richarlison anakwenda chini.
Mbrazil huyo alijishindia zawadi ya penalty kufuatia kusukumana na mlinzi wa Gunners, Hector Bellerin kitu ambacho Arsene Wenger ameita ni maamuzi ya kashfa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad