Ozil yuko mbioni kuondoka dirisha dogo la January na Gunners wanajaribu kusaka mteja - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Tuesday, 17 October 2017

Ozil yuko mbioni kuondoka dirisha dogo la January na Gunners wanajaribu kusaka mteja

Inter Milan waonyesha nia ya kutaka kumchukua, na tayari mkataba wake unaelekea kumalizika mwisho wa msimu huu.

Boss wa Gunners, Arsene Wenger hatimaye amekiri hadharani kwamba wanalazimika kuwauza Alexis Sanches na Mesut Ozil kwenye dirisha dogo la January kuliko kuwapoteza wakiwa huru.
Lakini bado wataendelea kujaribu kumuweka sawa Ozil ambaye wanaona bado wanauwezo wa kumshawishi aendelee kubaki kwenye uwanja wa Emirate.
Pia imetokea hali ya kukatishwa tamaa kutokana na tabia ya Ozil na hata uwezo wake uwanjani, hasa baada ya kipigo walichopokea kutoka kwa Watford Jumamosi iliyopita.
Arsenal wameweka mezani kitita chenye thamani ya £275.000 kama malipo ya wiki kwa Ozil lakini wakala wa mchezaji huyo ameikataa offer hiyo na kudai £350,000 huku mazungumzo ya pande zote mbili yakiwa bado yanaendelea kufanyika.

Kazi ya Ozil kwa Arsenal inaonekana sasa inaelekea ukingoni.

Wenger anaonyesha kutaka kuruhusu Ozil aondoke zake January.

Ozil aliwaka baada ya Arsenal kupoteza mchezo dhidi ya Watford.
Tatizo walilonalo Arsenal ni kwamba Manchester City wanashauku ya kumchukua Sanchez lakini hawajaonyesha nia ya kumhitaji Ozil.
Inter Milan wamekiri hadharani kwamba nia yao ni kupata saini ya Ozil na ndiyo maana sasa wanahangaikia suala hili sokoni.
Arsenal wamepata matokeo mazuri bila ya uwepo wa Ozil na utambulisho wake kwenye mchezo dhidi ya Watford ilikuwa ni ishara kuonyesha mwongozo na matokeo yake wakapoteza mchezo huo Vicarage Road.

Hana makali tena na mapenzi kwa timu kiasi hali hata hali yake kwenye vyumba vya kubadilishia nguo imekuwa tofauti, hakika siku zake pale Emirates zinaonekana kuhesabika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad