Senga: daktari wa ugonjwa wa kununa, kilaza mitandao ya jamii - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Sunday, 8 October 2017

Senga: daktari wa ugonjwa wa kununa, kilaza mitandao ya jamii

Na: Nsaji Lebhi

Mchekeshaji wa Bongo Movie, Ulimboka Kajumile Mwalulesya maarufu “Uli Senga” analalamikia maendeleo ya teknolojia kuwa yanatumika kama ngazi ya kurahisisha wizi kazi za wasanii hasa wa sinema na muziki.


Senga ametoa kilio chake alipoongea nasi kwa njia ya simu tulipotaka kusikia sababu ya yeye kutoonekana kwenye mitandao ya kijamii na mambo mengine kadhaa yanayohusu kazi yake ya sanaa kwa ujumla.
Anasema kuwa hachukii kuona dunia inabadilika kitenkolojia lakini matumizi yake kwa baadhi ya watu yamekuwa ya kiujanja sana kiasi cha kuathiri mapato ya wasanii kwa kiwango kikubwa kwasababu kazi zao zinaibiwa na kuhifadhiwa kisha nakala zinatengezwa na kuuzwa bei ya chini ambayo mhusika haambulii hata senti ya mauzo hayo.
Senga anasema kuwa serikali haipaswi kulaumiwa sana kwa hili hata kama zitatengenezwa sheria na kanuni kali za kusimamia biashara hii, isipokuwa jamii yenyewe ndiyo inapaswa kubadilika na kuunga mkono kazi zote ili kila mmoja apate kunufaika kwa nafasi yake.
Akiongelea issue ya yeye kutooneka kwenye mitandao ya kijamii senga anakiri waziwazi kuwa yeye hatumii na wala hana ujuzi wa kuitumia ila sasa anataka ajifunze kuitumia ili aendane na kasi ya dunia pamoja na kujiweka karibu na wateja wake.
Anasikitika sana na haungi mkono tabia ya watu wa Bongo Movie kuwekeana madaraja hasa kitendo cha wasanii wa vichekesho kugeuzwa kuwa walinzi na wafungua mageti kwenye filamu nyingi, anaeleza kwa lafudhi ya Kinyakyusa, “sifurahii kabisa hii hali……….tunatakiwa tushikamane sote, mimi na mdau wangu Pembe tuko pamoja na nakuhakikishia daima sisi tutafanyakazi pamoja, kuona tunatenganishwa kikazi ni sawa na kumtoa samaki majini.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad