Beyonce na Jay Z Watoka Nje na Mapacha Wao kwa Mara ya Kwanza - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Friday, 6 October 2017

Beyonce na Jay Z Watoka Nje na Mapacha Wao kwa Mara ya Kwanza

Blue Ivy akiwa sambamba na wazazi wake pamoja na wadogo zake Rumi na Sir Carter wameonekana kwa ya kwanza wakiwa kwenye mtoko wa kifamilia.
Ijumaa jioni wazazi hawa walionekana wakiwa wamewabeba watoto wao huku wakiwa wanaelekea kwenye maegesho ya helikopta mjini New York huku wakiwa wameambatana na walinzi wao, ilivutia sana macho ya wengi.
Jay Z akiwa amembeba mtoto wake
Pichani anaonekana Beyonce kwa mara ya kwanza akiwa na mumewe na watoto wake mapacha kwenye mtoko wa kifamilia.
Mkali wa ngoma ya “Formation” alikuwa amevalia mavazi yaliyomka mkaa vyema mwilini akiwa amebeba mkoba huku msaidizi wake akiwa nyuma yake amembeba mmoja wa mapacha kwenye kibebeo maalum cha watoto.
Jay Z ameeleza sababu iliyopelekea kuwapa watoto wake mapacha majina ya kipekee .
Pic Beyonce aliweka picha hii kwenye ukarasa wake wa Instagram siku watoto wake walipotimiza mwaka mmoja, July 14.
Akizungumza na Rap Radar jana Ijumaa namna walifikia kuchagua majina ya watoto wao, alisema, “Rumi ni mshairi tunampenda sana, …….tukaona ni vyema tumwite binti yetu jina hilo.”
Na alipomzungumzia pacha wa kiume, mzee wa 4:44 akaendelea kusema, “Ukisema Sir ni sawa na kusema mwanaume, kwahiyo amekuja huyu mwanaume…….na amekuja kiume.”
Jay Z pia hakuacha kumwongelea binti ya mkubwa “Blue Ivy” namna anavyoghani mashairi ya nyimbo za album yake ya sasa 4:44.

Anasema, “alivaa headphones akapanda kwneye stuli kasha akaanza kurap……..nikastaajabu sana, na ninayo video niliyomrekodi kwneye simu yangu…….dakika tano, dakika tano akifanya mambo yake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad