Van Gaal aponda namna Mourinho alivyompoka kazi yake Utd - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Monday, 16 October 2017

Van Gaal aponda namna Mourinho alivyompoka kazi yake Utd

Louis van Gaal amemzungumzia Jose Mourinho miezi 16 baada ya kung’olewa kwenye kiti cha umeneja Manchester United.
Mholanzi huyo akabaki anashangaashangaa alipokutakana uso kwa uso na Mourinho kwenye korido la Anfield, ambapo Mourinho akatumia nafasi hiyo kumkaribisha glass ya wine baada ya sare ya bila kufungana na Liverpool fc.
Kutokana na maelezo ya Van Gaal, ni kwamba Mourinho alimwita boss wake huyo wa zamani “mister”  na akajitahidi kuwa mwema kwake kadiri awezavyo.
Van Gaal anaamini kuwa bwana mdogo huyo wa kireno alikuwa anataka sana kupata kazi United hata angali yeye amekalia kiti cha ukuu pale Old Trafford.
Alisema, “Pasi na shaka, nilikuwa na wasiwasi juu ya hili, namna ya ajira yake ya umeneja wa Manchester United ilivyofanyika halikuwa jambo la kupuuza na kuchukulia poa kabisa. Hiyo ndiyo ilipelekea kufukuzwa kwangu.
Boss wa sasa wa United akisalimiana na mtangulizi wake kwenye uwanja wa Anfield Jumamosi ya October 14.
Kwa upande wa misingi ya kazi siyo mbaya. ni mtu mwenye ushirikiano na yuko hivyo siku zote hata wakati alipokuwa msaidizi wangu.”
Lakini mara nyingi huwa anashindwa kuimudu ghadhabu yake linapotokea la kutokea.”
Van alikaribishwa vizuri sana na watumishi wa klabu yake hiyo ya zamani pamoja na mashabiki na akaendelea kusema “Nimepata kumbukumbu nzuri sana na uhusiano wangu na watumishi pamoja na mashabiki ulikuwa safi tu wakati nipo United.”
Mholanzi Louis van Gaal alifurushwa vilago vyake Manchester United siku mbili tu baada ya kunyakuwa FA Cup.
Lakini mholanzi huyo aliyenyimwa kazi zaidi ya 20 mwaka jana, ataendelea kuwakumbuka mashabiki wa United ambao anaamini walikuwa ni kama kitu cha muujiza wanapofika uwanja wa Anfield.
Dakika kadhaa kabla ya filimbi ya mwisho kupulizwa, walikuwa wakiimba ’’’’’You’ll Never Walk Alone’’’’’’’’’….hii inanipa msisimko kwenye mwili wangu wote. Oh’ inapendeza sana,” aliongeza Van Gaal.
Meneja huyo mstaafu wa timu ya taifa ya Holland ameweka wazi kwamba alikuwa anapenda sana mchezo dhidi ya Liverpool kitu kingine chochote wakati alipokuwa United.
CEO wetu Ed Wood alikuwa ananiahidi chupa sita za Ribeiro Red Wine kila tukiifunga Liverpool. Nikashinda mara nne, hivyo nikawa na chupa nyingi tu,” akaendelea kusema kuwa “Huu ndiyo mchezo mkubwa kabisa Wingereza.”

Man City v Man United? Haiwezi hata kidogo kuisogelea ya Liverpool v Man United. Hii ni kubwa kama ya Real Madrid v Barca, au ya Ajax v Fayenoord nchini kwangu.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad