Jose Mourinho: Siku moja nitaeleza kwanini sikusaini Barcelona 2008 - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Monday, 16 October 2017

Jose Mourinho: Siku moja nitaeleza kwanini sikusaini Barcelona 2008

Mwaka 2008 Frank Rijkaard alipigwa panga, Mourinho alikuwa kwenye mbio za kushika usukani, lakini badala yake akatimkia Inter.

Huenda Jose Mourinho angetwaa ubosi wa Barcelona na kuiongoza timu hiyo ambayo wakati huo ilitawala soccer la dunia huku ikiwa na kikosi kilichosheheni vipaji vya hali ya juu.
Meneja huyo wa sasa wa Man United aliyeanzia kazi ya ukarimani na baadaye akawa kocha msaidizi wa Bobby Robison na kisha akaungana na kikosi kazi cha Louis van Gaal kwenye ofisi za Nou Camp maiaka ya 1990.
Lakini mpango wa kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo ungewezekana baada ya kupata mafanikio alipokuwa Porto na Chelsea ambako alibeba ubingwa wa Champions League na Premier League.
Mwaka 2008 Frank Rijkaard alipofukuzwa, Mourinho alikuwa kwenye mbiyo za kuiongoza Barca iliyokuwa na kikosi chenye vichwa vinavyoheshimika duniani kote akiwemo Lionel Mesi, Andreas Iniesta, Xavi Hernandez, Thierry Henry, Samuel Eto’o  sambamba na academic ya timu.

Mourinho alifanya kazi na Bobby Robison na Louis van Gaal kwenye dimba hili la Nou Camp.

Ni lini tutajua ukweli wa kilichotokea?

Badala yake, Pep Guardiola akaichukuwa Barcelona.
Lakini hakupata kazi na badala yake akatimkia Inter Milan ambako alifurahia mafanikio ya ligi ya Italia sambamba na yale ya Bara la Ulaya wakati huo Barcelona ikiendelea kung’ara chini ya Guardiola.
Haya mambo yanahusu kazi yangu ambayo binafsi naipa kipaumbele” alisema wakati akifanya mahojiano na Telefoot.
Labda nitakuja kulizungumzia hili siku moja nikiwa nimezeeka, tena nimezeeka sana.”
Kitu pekee nachoweza kusema ni kwamba mimi bado kocha mwenye matamanio na malengo ya kuja kufanya vitu vipya.”

Mourinho akaenda zake Inter badala ya Barcelona.
Nina hakika kazi yangu haitaishia hapa Manchester United. Kuna siku mwanangu anayeishi London, alienda Paris kutazama mchezo wa PSG na hakutaka kutazama wa Manchester.”

kwanini Paris? Kwasababu kuna vitu fulani maalum……..miujiza ya soccer, ubora, vijana…..iko poa kiujumla.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad