Paris Jackson binti wa miaka 19 aijia juu tweet ya Wendy Williams 53 - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Friday, 3 November 2017

Paris Jackson binti wa miaka 19 aijia juu tweet ya Wendy Williams 53

Binti wa mfalme wa pop duniani, hayati Michael Jackson ameshindwa kuvumilia na hatimaye kaamua kumchana yule mama maarufu kwa umbeya nchini Marekani baadaya mambo ya familia kufanywa mada kwenye mtandao wa tweeter.
Alhamisi ya jana Paris Jackson alijibu tweet ya bibi huyo wa miaka 53 iliyosema “mmelisikia songombingo jipya la familia ya Jackson?”
Paris Jackson alipohudhuria kwenye tukio Beverly Hills huko California Marekani mwezi uliopita
Tweet ya bibi mpekuzi ilikuwa na picha ya mama yake Michael Jackson, bi Katherine Jackson sambamba na ya mjukuu wake wa miaka 15 Prince Michael Jackson II (Blanket), ikiongelea issue ya familia yake hususani upande wa malezi na ikawa linked kweye Hot Topics Runtown.
Hii ni tweet ya Wendy William ikiuliza jambo la kizushi juu ya familia hii maarufu kabisa duniani

Paris akaona isiwe tabu hata mimi ninaweza kuandika kama wewe na neno lako siyo sheria akijibu mapigo ya mama mbeya, na maneno ya Paris kwa Kiswahili yanaenda hivi "ugomvi wako hauna maana na unaweza kusababisha madhara makubwa, ninahakika kuna wataalamu wengi wa akili unaweza kwenda kuwaona"
Paris naye baadaye kidogo akaongeza jibu lingine kwenye ile tweet huku post yake ikiwa na picha yenye mchoro wa msichana anayeelezea jambo kwa hisia huku akiwa ameinua mikono yake kana kwamba kuna kitu kinachoendelea lakini hakielewielewi vyema. Ni kama anatamani atokee mtu mwenye kumnyamazisha huyu mama aache kuiongelea hovyo familia ya hayati Michael Jackson.
Inaonekana Mungu amechoshwa na upuuzi wake akaamua kumwonjesha joto ya jiwe kidogo kwa kutoacha kuyasema majina ya watoto wa watu
Kaka mkubwa wa Paris, Prince Jackson mwenye miaka 20 alipata ajali ndogo ya pikipiki jana asubuhi alipokuwa anaelekea chuoni kwake Loyola Marymount University karibu na Playa Vista.
Prince alishindwa kuimudu pikipiki yake wakati wa mvua hivyo akabebwa kwenye gari ya wagonjwa na kukimbizwa hospitali ambako hakuonekana kuwa na majeraha makubwa, kulingana na taarifa ya TMZ.
Wendy William, mama mtata mpekuzi, mbeya na mzungumza mambo ya watu
Michael Jackson ameacha watoto Paris na Prince aliozaa na Debbie Rowe ispokuwa huyu Prince Michael II teknolojia ya upatikanaji wake bado haifahamiki.
Paris anatarajia kuachia kazi yake ya filamu inayosimamiwa na mwongozaji kutoka Australia, Nash Edgerton mwenye miaka 44, inafahamika kama Gringo na itawahusisha David Oyelowo, Joel Edgerton, Amanda Seyfried na Charlize Theron itaingia sokoni March 9, 2018.
Baba na wana: Paris na kaka yake Prince wanaonekana wakiwa na baba yao jijini London mwaka 2005



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad