“Usiku mchungu Wembley” – Namna vyombo vya habari Hispania vinazungumzia kichapo cha Real Madridi kutoka kwa Tottenham - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Thursday, 2 November 2017

“Usiku mchungu Wembley” – Namna vyombo vya habari Hispania vinazungumzia kichapo cha Real Madridi kutoka kwa Tottenham

Mabingwa wa UEFA wameshuka kwa mara ya kwanza uwanja wa Wembley na kusambaratishwa vibaya na kikosi cha maangamizi cha Mauricio Pochettino

“Beware The Blacklish” ulikuwa ni ujumbe kwa Tottenham Hotspurs kuelekea usiku wa Jumatano ya jana, baada ya kipigo cha kushtusha alichopokea Real Madrid toka kwa Ginora weekend iliyopita.
Mabingwa hawa wa ligi kuu Hispania na Klabu Bingwa Ulaya msimu uliopita waliambulia patupu mchezo wao wa Jumapili kwenye La Liga.
Walidhamiria kuutumia vyema usiku wao wa kwanza kabisa kwenye dimba la Wembley nchini Uingereza lakini haikuweza kuwa kama walivyotaka.
Na badala yake, kikosi cha Zinedine Zidane kilishindwa kabisa kufurukuta na hatimaye kuambulia kichapo cha mbwa mdokozi huko kaskazini-magharibi mwa jiji la London.
Ronaldo alifunga goli lakini timu yake ilipigwa vizuri sana
Spurs walikuwa hawashikiki
Namna ubao ulivyokuwa ukisomeka
Dele Alli alitumbukia nyavuni mara mbili na Christian Eriksen naye pia akatumbukia nyavuni na kuwafanya vijana wa Mauricio Pochettino watoke vifua mbele kwa ushindi wa 3-1, lakini cha zaidi siyo kilichowatokea Real Madrid, hapa tuangalie namna vyombo vya habari vya Uhispania vinavyolijadili hili la vipigo viwili kwa Madrid ndani ya siku nne tu…………..Na lawama zinazoelekezwa kwao.
Gazeti la AS

Kichwa cha habari: Usiku wa Majinamizi Wembley
AS waliweka kichwa hiki cha habari kwenye ukurasa wa mbele sambamba na picha ya walinzi waliochoka kabisa wakingozwa na Sergio Ramos, Nacho na Kipa wao Kiko Casilla wakati mpira unatinga nyavuni mwao.
Ndani yake Javier Silles anaandika kwamba kikosi kazi cha Zidane “Hakika Hakifanyikazi Sawasawa” pande zote sasa zimedhoofu kuanzia ulinzi, viungo na washambuliaji hawafanyi lolote la maana kwasasa, kitu ambacho kimetafsiriwa kama kichapo cha maafa kutoka kwa Spurs.
Viungo wawili machachari Luka Modric na Toni Kroos wamekosolewa sana kwa kupoteza umiliki wa mipira mara 28 katika eneo lao kiasi kilichopelekea Kroos kuangushiwa mzigo wa matatizo yanayowakabili Real Madrid kwasasa.
Tomas Roncero anamlenga Karim Benzema, “mshambuliaji wa kwanza katika historia ya Real Madrid asiyeonekana kuhitaji kufunga magoli.”
Gazeti la Mundo Deportivo

Kichwa cha habari: Mtazamo wa Madrid
Katika kulichanganua tukio la jana usiku, gazeti hili la Mundo Deportivo lenye makao yake Barcelona limeandika Los Blancos “sasa wanaporomoka.”
Manuel Bruna anasema kwamba “Madrid hawana la kujitetea” na vijana wanaonekana wamechoka, ni Isco peke yake anayeng’ara kwa kila kitu, na kuongeza kuwa “Pochettino amemfunza Zidane somo la kiufundi.”
Josep M. Artells anaandika kwamba “Casemiro alikuwa amekumbwa na maafa, Kroos ni kama hakuwamo uwanjani na Modric alikuwa tepetepe…....Pochettino akamkonyeza Florentino akiashiria kuwa wamemmaliza mpinzani.
Delle Alli naye alikuwa na njaa kali baada ya kutupia kambani mara mbili, “alisababisha hofu kuu.
Gazeti la Marca

Kichwa cha habari: Piga Alarm Zote
Huku wakitumia picha kama ile ya gazeti la AS, Marca hawakutumia maneno yenye hisia kali……walichosema ni “Usifanye Makosa” lakini kinadharia huu ni ukosoaji, na ndani yake wanasema.
Harry Kane aliachiwa huru na sifa zimwendee kwa kuyatimiza vyema majukumu yake yaliyowapatia ushindi mnono nyumbani ingawa hakufunga. “Hivi Real Madrid hawatafuti mchezaji namba 9? Kwasababu baada ya kumwona Kane, basi watume skauti wao waende pande yoyote ya dunia lakini isiwe Wembley kwa maana itakuwa ni kupoteza muda na pesa. Harry ni mwanaume wa soka.
Hugo Cerezo anaweka wazi kwamba “mchezo mbaya kabisa katika nyakati hizi za Zidane” na yeye anathibisha kuwa ni Isco pekee aliyekuwa hai kwenye mchezo huu.” Anaongeza, “kofi la uso haliji kwa mbabe wa Ulaya,lakini ni mchezo wa marudiano bila ya ushindi kwenye klabu bingwa Ulaya.”
Gazeti la Sport

Kichwa cha habari: Hakuna Malengo
Gazeti hili pia linatokea jijini Barcelona, kwenye picha anaoneka Cristiano Ronaldo amevurugwa vibaya sana huku mikono yake ikiwa kiunoni na amepoteza nuru ya uso wake wakati huohuo wanonekana wachezaji wa Spurs wanashangilia kwa furaha pamoja.
Matatizo yanazidi kuota mizizi kwa Madrid” anaandika Ivan San Antonio, anyethibitisha kuwa Delle Alli kiungo wa kiingereza anayekuja na makali mithili ya moto wa kuyeyushia chuma.

Sifa nyingine anaelekeza kwa wakali hao wa kaskazini mwa London . “Tottenham walielekeza nguvu yao ya pamoja kwenye mchezo huu mgumu, bila kupumzika, hawakuwa na muda wa kufikiria wala kuvuta pumzi,” anaongeza “Tottenham kiukweli walicheza mpira…….lilikuwa jiwe zito kwa Real Madrid.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad