Christian Atsu wa Newcastle anamsaka mtu aliyebadili maisha yake ya soccer - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Thursday, 5 October 2017

Christian Atsu wa Newcastle anamsaka mtu aliyebadili maisha yake ya soccer


Atsu alihangaika sana kujiaminisha apate namba ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Chelsea bila mafanikio, lakini sasa amekuwa kivutio kikubwa Tyneside baada ya kusaini mkata wa uhamisho wenye thamani ya paundi milioni sita.
Bado anakumbuka tukio la wema aliotendewa wakati alipokuwa bado kinda na kuifanya ndoto yake kuwa hai.
Alikulia kwenye kijiji cha Ada Foah, kilicho mwendo wa saa  moja kutoka mwambao wa Accra, mji mkuu wa Ghana. Alikuwa mcheza mwenye uwezo mkubwa wa kulitandaza soccer tangu utoto wake, akicheza kwenye viwanja visivyo na nyasi huku vikiwa vimejaa mawe madogodogo kibao.
Siku moja kabla mashindano ya majaribio yaliyoandaliwa na Fayenood’s West African Academy, mtu mmoja asiyefahamika kabisa kutoka Achimota Accra alimpatia viatu vipya vya soccer.
Alivivaa, akajisikia vyema kabisa, akacheza vizuri sana na hatimaye akaanza rasmi harakati za kwenda kucheza ligi kuu ya Wingereza akipitia timu ya Uholanzi na FC Porto ya Ureno.
Walininunulia viatu bwana kwasababu walikuwa wanasema nina kipaji na lazima nikifanyie kazi,” alisema Atsu alipokuwa anafanyiwa mahojiano kwenye eneo la mazoezi uwanja wa Newcasctle. “Kwakweli hii kitu sitaisahau kamwe.”
Christian Atsu, anatafuta namna ya kurudisha fadhira za wema aliotendewa

Kulikuwa na watu ambao walikuwa hawafahamiki na walikuwa wanataka niendelee kufanya vizuri. Watu wa mji nilikokulia wakiona unakipaji kuna wakati watakupatia pesa ya kukusaidia, au chakula ili kikujenge n ahata viatu pia.
Hivi ndivyo watu wa Afrika wanapenda soccer, watu usiowafahamu kabisa! Hivyo ndivyo afrika ilivyo. Na hiyo ni roho ya kijumuia unayoweza kukutana nayo uwapo Afrika.”
Wanakuona, wanakufanya uwe na furaha na watataka kukusaidia.
Mapema mwaka huu Atsu alianza kumfikiria mtu aliyemtendea wema, ni baada ya Newcastle kumpandia dau la kumnunua kutoaka Chelsea kwa paundi milioni sita.
Atsu wakati wa mchezo wa Huddersfield Town vs Newcastle United

Anaendelea kusema “Nilitaka sana kumwona mtu huyo, nikampanga rafiki yangu amtafute, alikuwa anaitwa Joshua. Ni mtu mwema sana.
Alinunua viatu na sikuwahi kumwona tena. Sasa nimekuwa na ukaribu naye lakini hataki chochote kutoka kwangu, lakini nilitaka japo nafasi hata kusema asante.
Kuna sababu inayompeleka Atsu nyumbani kila wakati wa mapumziko. Mwaka huu alibeba mzigo wa jezi na viatu vya Newcastle Unite pamoja na pipi na kuwapelekea watoto katika kituo cha kulelea watoto yatima.
Mwezi June mwaka huu alitembelea na kutoa zawadi mbalimbali kwenye kituo cha kulea watoto yatima kijijini kwake

Atsu alipmpoteza baba yake mzazi akiwa na umri miaka 13 na mmoja wa ndugu zake 11 wa kuzaliwa.

Anaendeleza gurudumu la kutoa kwa jamii ambalo limemsaidia yeye kufika hapa alipo sasa.
Akishangilia baada ya kuweka mpira nyavuni kwenye wa Sept 16, 2017 kwenye mchezo baina Newcastle United na Stoke City

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad