Ni dogo wa miaka 14
lakini sasa anatambulishwa kama David Beckham mpya na jina lake limeanza
kutamkwa mara kwa mara kwenye viunga vya Manchester United.
Kwasasa Phil mtoto yupo
miongoni wachezaji wa timu ya watoto ya Valencia inayojulikana kwa jina la Los
Ches, na anafananishwa na Beckham kwasababu ya uwezo wake mkubwa wa kutumia guu
la kulia kupiga mipira mirefu yenye macho.
Harvey Phil Neville
aliingia Valencia mwaka 2015 baada ya baba yake kuteuliwa kuwa msaidizi wa kocha
mkuu Gary Neville ambaye ni baba yake mkubwa. Lakini baba zake walifurushwa nje
ya La Liga baada timu kufanya vibaya.
![]() |
| Harvey Neville yuko kazini |
Hata hivyo Harvey
alisalia nchini Spain baada ya kupatiwa mkataba mpya na sasa uwezo wake
umeimarika na kuwa moja ya wachezaji chipukizi bora kabisa.
![]() |
| Kocha wa timu ya vijana ya Manchester United, Eric Harrison akiwa na wachezaji wake Ryan Giggs, Nicky Butt, David Beckham, Gary Neville, Phil Neville, Paul Scholes na Terry Cooke, 1992. |
Na sasa chombo cha
habari nchini Spain maarufu kama Super Deporte kinaripoti kwamba Man U wako
katika mkakati wa kmrejesha nyumbani alikokulia baba yake.
![]() |
| Harvey Neville akionyesha namba ya fulana yake Valencia |
![]() |
| Dogo anapata umaarufu nchini Spain |
Inasemekana hata
Tottenham Hotspurs wanamuwania Harvey Neville.
Harvey alianza maisha
ya soccer kwenye timu ya watoto ya Carrington baadaye akaenda Manchester City
kabla familia yake kuhamia Spain.
![]() |
| Harvey ataweza kupita vyema nyayo za baba zake? |
Baba yake “Phil Neville”
anajivunia sana maendeleo ya mwanae kiasi amekuwa na utaratibu wa kurekodi na
kurusha mara kwa mara video za mwanae akiwa na timu yake ya Valencia kiasi cha kukamata
hata macho ya David Beckham kwenye kurasa yake ya Instagram.
![]() |
| Phil Neville na familia yake |






No comments:
Post a Comment