Lionel Richie “anayaogopa mahusiano ya bintiye na Scott Disick” - SPORTSTAIN

SPORTSTAIN

Stay with us. Be informed

Thursday, 5 October 2017

Lionel Richie “anayaogopa mahusiano ya bintiye na Scott Disick”

Mkongwe wa muziki nchini Marekani, Lionel Richie anatamani amzuie  bintiye wa miaka 19 kutoka kimapenzi na mkali wa bata za kimataifa Scott Disick.


Lionel Richie ameshindwa kuzuia hisia za anachofikiria juu mahusiano hayo ya bintiye na bwana Scott.
Sofia ana miaka 19 na huyo baba wa watoto watatu mwenye miaka 34, juzi kati walionekana hadharani wakiwa kwenye mtoko wa nguvu na kuuthibitishia ulimwengu kuwa wanatoka kimapenzi na wameshibana sana tu.
Lakini mzee wa “All Night Long” ameweka wazi kuwa yeye anawasiwasi sana na mahusiano hayo.
Nimekuwa na hofu?.........mimi ni baba,……….wacha kabisa bwana,” aliongea hivyo alipozungumza na US Weekly.

Richie na Sofia
Rich na Sofia miaka ya hivi karibuni

Alipoulizwa kama yuko poa kuyakubali mahusuano hayo, akasema: “ninaogopa kiasi nahisi kufa……….unanizingua au siyo?”
Sofia na Scott walifotolewa mapicha wiki hii wakiwa wamejituliza PDA nchini Mexico kama njia ya kufurahia penzi lao jipya.
Baba wa watoto watatu  na binti mwanamitindo waliyaanika mapenzi yao hadharani kwa video waliyojirekodi wakikisi wiki kadhaa zilizopita na baadaye wakaonekana wakitumbukia kwenye maji na kuogelea huku wakiwa na furaha iliyopiliza.
Chanzo cha habari cha awali kiliwaambia watu kuwa Sofia Richie amemkubali sana Scott.

Scott Disick na Sofia Richie

Wambeya nao hawako nyuma, wanasema kuwa Scott na Sofia hawakai mbali, muda wote wanakuwa pamoja.
Scott anampetipeti sana Sofia, anamfungulia mlango wa gari na analipia kila kitu kwa Sofia” walidai wananzengo.
Sofia Richie
Scott Disick

Scott ameshawahi kuwa kwenye mahusiano na wanawake kadhaa tangu alipoachana na aliyekuwa kuwa mke wake mwenye watoto wake watatu Kourtney Kardashian, mwaka 2015.
Kuna wakati alihusishwa kuwa mahusiano na mcheza sinema Bella Thorne, ambaye inasemekana kuwa ana umri kama wa Sofia.


Habari hii imetafasiriwa na Davis Mwakalosi kwa hisani ya mtandao Mirror. Tafadhari wasiliana nasi kwa njia ya email sportstz17@gmail.com au tembelea, ku-like na ku-follow account zetu za Facebook  (sportstain), Instagram (sportain_tz) na Tweeter (sportain_tz).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad